PICHANI: ni mabaki ya ndege aliyokuwa amepanda mheshimiwa Akukweti baada ya kupata ajali katika kiwanja kidogo cha ndege jijini Mbeya.

Siku chache baada ya moto uliounguza “mikoba” ya waheshimiwa fulani fulani pale Mwanjelwa, na mali zenye thamani ya mamilioni ya shilingi za Kitanzania kwa baadhi ya wafanyibiashara, akaja Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Bunge, Mheshimiwa Juma Akukweti, si akaja Mbeya kuona ukubwa wa madhara yaliyotokana na moto huo na kisha kuwapa pole waathirika wa janga hilo!!!

Alipokuwa anataka kuondoka siku hiyo jioni hali ya hewa ikakataa, haikuruhusu apae na ka-ndege kake, akalazimika kuondoka alfajiri ya kesho yake yaani siku ya Jumamosi ya tarehe 16/12/2006. Kwa bahati mbaya sana akakumbana na dhahama la aina yake, ka-ndege kake kakashindwa kumudu kuruka, kakaenda kuvamia nyumba za wakazi zipatazo tatu na kulipuka.

Mungu epushia mbali, mheshimiwa akanusurika japo alipata majeraha yenye kumpa maumivu makali hasa sehemu za kichwani, na yeye na timu ya waliokuwa kwenye ndege hiyo wakawahishwa hospitali ya rufaa ya mkoani Mbeya kwa matibabu.

Kweli uswahilini noma, unajua wazushi wakaanza kudai huko mitaani eti jamaa hakutoa pole bali kuwabeza waathiurika wa moto ule kwa kuwaambia “Tulishawaambia mhame hapa lakini”, kwahiyo?? Huku uswahilini wanadai eti ajali ilitokana na chuki za wakazi aliowapa ukweli kuwa walishaambiwa wahame hawakusikia ndio maana moto ukawafanya kitu mbaya.

Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya mwandishi mwenzangu Theresia Nyantori, wa idara ya Habari na Maelezo (au porojo?), aliyepoteza uhai wake katika ajali hiyo.

i{content: normal !important}i{content: normal !important}i{content: normal !important}