Ilianza katikati ya wiki kama masihara vile, wakati woko kuu na kubwa mjini Mbeya na lililo maarufu pia lijulikanalo kwa jina la Mwanjelwa lilipowaka moto  na maduka yanayokadiriwa kufikia 500 hivi, (Hata city hawana uhakika maana yalikuwa yakiibuka kila uchao bila hata vibali), na mali zinazokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya bilioni tano zikiteketea katika moto huo.

Siku hiyo hiyo katika eneo la Iyunga, kilomita zaidi ya tano toka Mwanjelwa, noto ulilipuka yalipo maghala ya Cocacola. Na katika eneo la Mama John, kama km moja na nusu toka mwanjelwa, watoto wawili walipoteza maisha kutokana na hitilafu zilizotokana na umeme.

Ajabu sasa ni siku ya pili yake, ambapo jamaa wanaosadikiwa kuwa na asili ya kabila la Ukinga, eti walikuwa wakilia sio kwa kuunguliwa na mali zenye thamani ya mamilioni ya fedha, bali kwa kuunguliwa na “mikoba” yao. Ama kweli vilio hutofautiana. Wengine wanalilia fedha na mali zao walizokuwa wamefungasha kwa ajili ya wateja wa krismass, wengine wanalilia Mikoba yao iliyoungua!!! Ni vituko Uswahilini.
Ajabu sasa i{content: normal !important}i{content: normal !important}i{content: normal !important}