Unadhani ingekuwa vipi?

Kama siku moja Mungu akiamua kuyafumua mapaa ya nyumba hapa duniani wakati wa usiku wa manane? Na unadhani ingekuwa vipi ikiwa katika hali ya nyumba hizo kuwa wazi kwa juu, Mungu akashusha nuru ya ghafla japo kwa dakika kama tano tu hivi kusudi muone kinachotokea ndani ya nyumba za watu usiku huo wa manane?

Ingekuwa vipi kama vijana wa Kitanzania wangeamua kwa dhati kabisa kuacha kushinda vijiweni wakikoka ganja na badala yake wakawa wanashinda katika viunga vya mahakama wakisikiliza uendeshaji wa kesi mbalimbali?

Ingekuwa vipi siku Sirikali ikiamua kuhalalisha bangi na kupiga marufuku sigara? Unadhani bei ya bidhaa hiyo ingekuwa kubwa na kuzidi kuwatajirisha wanaoifanya kwa kasi kubwa kiasi cha sasa?

Ingekuwa vipi Sirikali ingehalalisha Gongo na kupiga marufuku bia tulizozizoea kwa sasa? Unadhani vifo vinavyotokana na Gongo vingepungua kwasababu vingi vinatokana na wahusika kuinywa kwa kuikomoa kwakuwa kesho wanaweza kuja wakakuta mama muuza yuko Lupango?

Ingekuwa vipi kama Sirikali ingeamua kuwa kuanzia sasa mabadiliko yote yatakuwa yakifanyika kuanzia vijijini kuelekea mijini na sio kinyume chake? na unadhani Ingekuwa vipi kama leo nisingekuuliza Ingekuwa Vipi?…….. UTAJIJU!!