Kuna mambo kadhaa ya muhimu sana ambayo yanajiri katika Ulimwengu wa Ma-Bloga kwa ujumla ambayo ni vyema kila mmoja akayajua. Kupitia kwa Bw. Ndesanjo Macha, nimekutana na taarifa za kuwepo kwa Siku ya Kublogi Duniani au pia waweza kuiita Siku ya Wana-Blogi Duniani. Soma zaidi kuhusu siku hiyo kwa Kiswahili HAPA. Pia soma juu ya aliyeanzisha wazo hilo HAPA.
*****************
Pia kuna Taarifa ambayo Mtanzania huyo amemaliza kuiandika kuhusu Wana-Blogi mbalimbali nchini na hata walio nje ya nchi (wenye asili ya Kitanzania, bilashaka) ambayo mnaweza kuisoma kwa kuingia katika blogi ya Sauti za Dunia (blogi ya Global Voices). Kwa mara nyingine tena, Bw. Ethan anazungumzia juu ya Wana-blogi flani flani hivi na ni vyema mkapata kile anachokisema HAPA