Nazungumzia Bunge letu tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambalo kwakweli hivi sasa kuna watu wamekuwa wakijitahidi kwa kadiri wawezavyo kuhakikisha kuwa wanaufuta utukufu wake na badala yake kulifanya sehemu ya kupotezea wakati. Na HII HAPA ni moja ya kazi nyingi sana ambazo ninatarajia kuwa wasomaji wangu watashirikiana nami katika kuibua hoja za msingi kabisa za kurekebisha baadhi ya mambo ambayo ni wazi kabisa yanaenda kombo.