Kwa haraka haraka, wapo wale wenzangu na mimi ambao watakuwa wameshangazwa kama sio kushtushwa na matokeo haya, lakini ndio hivyo tena. Hayawi hayawi, hatimaye yamekua. Inawezekana kuwa yalikuwa Maajabu, kama yale ya mzee Rajabu ya kushangaa kababu akavikwa hijab, lakini ukweli utabakia palepale kuwa ndio waliopita na WENYE WIVU WAJINYONGE TU, ila wenzenu haoooooooooo, wanaingia Bungeni pale (sijui kwenda kusinzia sawa na wenzao au vipi, tuwaachie wenyewe hayo).

Kwa kutizama sifa zao tu, hakika wanastahili hicho walichokifikia. Nawazungumzia ndugu zangu hawa wawili ambao majuzi wamefanikiwa kuteuliwa kuwa wawakilishi wa vijana katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nawazungumzia Amina Chifupa Mpakanjia na mwenzake (katika uwakilishi) Lucy Thomas Mayenga. Kwa kweli kama ni kutosha kura zilitosha, lakini je ndio upele umempata mwenye kucha kweli,au kucha zimempata mwenye upele???