Kwa haraka haraka, wapo wale wenzangu na mimi ambao watakuwa wameshangazwa kama sio kushtushwa na matokeo haya, lakini ndio hivyo tena. Hayawi hayawi, hatimaye yamekua. Inawezekana kuwa yalikuwa Maajabu, kama yale ya mzee Rajabu ya kushangaa kababu akavikwa hijab, lakini ukweli utabakia palepale kuwa ndio waliopita na WENYE WIVU WAJINYONGE TU, ila wenzenu haoooooooooo, wanaingia Bungeni pale (sijui kwenda kusinzia sawa na wenzao au vipi, tuwaachie wenyewe hayo).
Kwa kutizama sifa zao tu, hakika wanastahili hicho walichokifikia. Nawazungumzia ndugu zangu hawa wawili ambao majuzi wamefanikiwa kuteuliwa kuwa wawakilishi wa vijana katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nawazungumzia Amina Chifupa Mpakanjia na mwenzake (katika uwakilishi) Lucy Thomas Mayenga. Kwa kweli kama ni kutosha kura zilitosha, lakini je ndio upele umempata mwenye kucha kweli,au kucha zimempata mwenye upele???
August 18, 2005 at 9:29 pm
Eh bwana ee, Chifupa kashinda ila sina hakika kama ana uwezo kitaaluma unaoendana na dunia ya kileo.Kwa hiyo kama ni kusinzia nafikiri ndio walewale.
Nafikiri ni tamaa ya pesa na ujiko ndio vilivyomshindisha bila shaka.Sina wivu ila kwa ninavyomjua nimemfuatilia ktk kazi yake ya utangazaji sikuwahi kumsikia akianda kipindi makini yaani issue nzito nzito kuhusu mustakabali wa nchi yetu.
Tusubiri tumwone,ila ana kimbola cha kashfa asipoangalia kitamuandama zaidi sijui awape nini wanahabari wamstahi.
August 18, 2005 at 11:11 pm
Nadhani wengi hupendelea vitu ambavyo si makini ndi maana amekwaa umaarufu mkubwa namna hiyo hadi ubunge. Kwa usanii wa bunge letu kila mtu anaweza anyway!!
September 4, 2005 at 12:58 pm
Ni kwela uyasemayo maan ndani ya kipindi cha uchaguzi tu Amina Chifupa wa Mpakanjia alilopoka nasema kulopoka maana pale si mahala pake kwa maneno kama kasheshe, alipoambiwa tu achague wa kumsimamia kura akasema kasheshe sasa kwa maoni yangu nashindwa kuelewa je huko bungeni itakuwaje? maana tabia haina dawa ingawa tunambiwa ameanza kujirekebisha lakini alikuwa wapi kujirekebisha tangu akiwa form two kwani inasemekana alifukuzwa shule kwa utovu wa nidhamu pale jangwani.
Ila tumuachie spika kazi hiyo analo la kumrekebisha tabia binti yule na je vile vijisuruali vya kubana atavivalia wapi na je pochi yake ina sehemu ya kubebea vitabu vya maswali na majibu kama si atajaza vipodozi kama kwaida yake kaka tutaendelea kesho Tchao
September 4, 2005 at 12:58 pm
Ni kwela uyasemayo maan ndani ya kipindi cha uchaguzi tu Amina Chifupa wa Mpakanjia alilopoka nasema kulopoka maana pale si mahala pake kwa maneno kama kasheshe, alipoambiwa tu achague wa kumsimamia kura akasema kasheshe sasa kwa maoni yangu nashindwa kuelewa je huko bungeni itakuwaje? maana tabia haina dawa ingawa tunambiwa ameanza kujirekebisha lakini alikuwa wapi kujirekebisha tangu akiwa form two kwani inasemekana alifukuzwa shule kwa utovu wa nidhamu pale jangwani.
Ila tumuachie spika kazi hiyo analo la kumrekebisha tabia binti yule na je vile vijisuruali vya kubana atavivalia wapi na je pochi yake ina sehemu ya kubebea vitabu vya maswali na majibu kama si atajaza vipodozi kama kwaida yake kaka tutaendelea kesho Tchao
September 4, 2005 at 12:58 pm
Ni kwela uyasemayo maan ndani ya kipindi cha uchaguzi tu Amina Chifupa wa Mpakanjia alilopoka nasema kulopoka maana pale si mahala pake kwa maneno kama kasheshe, alipoambiwa tu achague wa kumsimamia kura akasema kasheshe sasa kwa maoni yangu nashindwa kuelewa je huko bungeni itakuwaje? maana tabia haina dawa ingawa tunambiwa ameanza kujirekebisha lakini alikuwa wapi kujirekebisha tangu akiwa form two kwani inasemekana alifukuzwa shule kwa utovu wa nidhamu pale jangwani.
Ila tumuachie spika kazi hiyo analo la kumrekebisha tabia binti yule na je vile vijisuruali vya kubana atavivalia wapi na je pochi yake ina sehemu ya kubebea vitabu vya maswali na majibu kama si atajaza vipodozi kama kwaida yake kaka tutaendelea kesho Tchao