Ingawa bado Chama tawala nchini Tanzania hakijatangaza rasmi kile watakachokiita ilani yao ya Uchaguzi mkuu kwa mwaka huu wa 2005, kuna jambo mojambalo limejitokeza wazi, nalo ni kuwa tayari wameshakuwa na kitu wanachokiita KAULI MBIU YAO ambayo ni Ari mpya, Nguvu mpya na Kasi mpya. Jambo moja tu ambalo bado linanitatizo hapa ni kuwa hivi hiyo kasi ni ya kuelekea wapi maana hawajatueleza kuhusu hilo?

Hivi tunajua kuwa kukimbia sio lazima kuwe ni kwa kwenda mbele, bali hata nyuma na kama ni hivyo kwanini hawa jamaa zetu wasituwekee hili wazi kuwa ni kasi ya kuelekea wapi???