Makala hii itakuwa ni moja kati ya kazi zangu nyingi sana ambazo zitakuwa zikiwagusa kwa undani sana vijana (wenzangu wa CCM, wanajua namaanisha hadi umri gani), kuhusiana na maisha yao ya kila siku na hasa katika harakati zao za kila siku za kupambana na gonjwa harati la UKIMWI.
Pamoja na mambo mbalimbali yatakayokuwemo katika kona hii, pia katika siku za karibuni utaweza kukutana na historia yangu kwa undani kiasi chake na nini hasa nimeweza kufanya katika harakati za kupambana na ukimwi. Je wajua kwanini niliamua kwenda kupima na unajua kuwa matokeo yangu yalikuwaje?, Basi kaa tayari kwa ajili ya kusoma kazi hii hivi karibuni.
Wakati tukiwa tunasubiri kwa hamu kazi hii, naomba tuendelee na kazi ambazo ziko tayari tukianzia na hii hapa.