papa
Huyu ni hayati Baba Mtakatifu, John Paul II, ambaye katika enzi za uhai wake, siku chache sana kabla hajatangulia mbele za haki, aliwahiwashangaza sana baadhi ya waumini na wasio waumini wa Kanisa katoliki kote duniani, kwa kusimama hadharani na kuomba msamaha kutokana na makosa mbalimbali ambayo alisema kuwa kanisa limeyafanya kwa kipindi kirefu yasiyokuwa ya kimaadili na ambayo yalikuwa yakiiumiza jamii na (bilashaka), kuliweka kanisa katika hali tata.

Inawezekana kabisa kuwa wengi kati ya waliomsikia akisema hayo, hawakujua kuwa alimaanisha nini, lakini ushahidi kuwa kweli mambo hayo yalikuwepo na kwamba sio ajabu kuwa yataendelea unazidi kujionyesha wazi wazi. Unajua ni kwanini? Soma hapa na kisha utoe maoni yako kuhusiana na hili.