tumeshinda

Hakika kila achekaye mwisho hucheka sana, sijui kuwa ilikuwa siku ya kufa nyani, miti yooote ikawa inateleza au yalikuwa yale ya “Yakhe, kufungwa twafungwa lakini vyenga twawala”, sijui kwakweli jambo moja ninalojua na ambalo nina uhakika nalo ni kuwa tumebeba kombe la FA, tena sio hivyo tu, bali pia tumelibeba toka mikononi mwa Manchester United. Poleni mlioumia