Ninachomaanisha hapa ni Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, ndugu zangu. hakika ni juhudu kubwa sana ambazo zimekuwa zikifanywa na Watanzania katika kuhakikisha kuwa walau tunaongeza kasi ya kuwafukuzia wenzetu ambao tayari walishatutangulia maili kadhaa siku zilizopita. Baada ya kuwepo kwa Watanzania kadhaa ambao wamekuwa wakiblogu katika lugha ya Kiswahili, hivi sasa wameamua kuanza kubobea zaidi kwa kutumia lugha za makabila ya Kitanzania. Kwa kuanzia, yupo binti aliyeko Marekani, ambaye ameamua kublogu klwa kutumia lugha ya Kichaga. Huyu ni ANNETH ASSENGA. Hebu msome hapa
.
May 23, 2005 at 10:27 am
wawa Ngoja kwanza nianze kufagiliaa kwa kichaga kwa kuwa aliye anzaa kuandika kiluga ni Mtani wangu weee omiiiii Jamani anasahaili pongezi manaa unajuwa tena wenzetu mbona wanatafsiri katika Lugha zao siunajuwa ena unapandishaia chati na watu wanaanza kujuwaa kuwa he kumbe kuna kabila hili ulimwenguni na kufanya watu wawe na hamu yakujuwaa je hawa watu ni wa aina gani wako wapi na mambo kama hayoo du sasa nisadiee kuwambiaa huyo Binti kuwaa jaribu kufagilia kuwa hata anapotoka yani mkoani kwake ndio kuna kilima Kiaro (Kilimanjaro)
Hiyo yawesa leta watalii atii