Kutoka 'Kilimanjaro' hadi 'Kilimachao'
Hii ni sehemu ya kilele cha Mlima ambao awali sio tu kwamba ulikuwa umefunikwa kwa theluji kwa zaidi ya asilimia 75 ya eneo lake, bali pia rasilimali muhimu sana kwa Watanzania, rasilimali ambayo ingeliweza kulifanya taifa hili kuvuna mabilioni ya Dola kupitia mlima huu.
Lakini dah!, yaliyoupata mlima huu ni makubwa mno. Sio tu kuwa Watanzania tulishindwa kabisa kuudhihirishia ulimwengu kuwa mlima huu ni wetu (uko Tanzania), bali pia tumeshindwa kuutunza hadi theluji iliyokuwa imeufunika imebakia kuwa sehemu ya masimulizi ya kale. na unajua nini, sio ajabu miaka kadhaa ijayo ukajasikia kuwa mlima huo kakabidhiwa mwekezaji ili auendeleze kwa maana sisi tumeshindwa.
Alahaula jamani