Kuna mmoja kati ya wasomaji wangu aliye Canada ambaye aliniuliza kuwa ni namna gani anaweza kunipata pamoja na kuhitaji pia kutambua vizuri Tanzania iki namna gani. Kwa manufaa yake yeye binafsi pamoja na wengine wote ambao bado walikuwa hawaijui vyema Tanzania, nimeanzisha kolamu maalum kwa ajili ya kuwawezesha wasomaji wangu kutambua baadhi ya mambo ya msingi kuhusiana na nchi yangu. naamini kuwa wakishamaliza kusoma hapo watakuwa katika nafasi nzuri ya kuweza kuja nitembelea au hata kutalii Tanzania. Karibuni Tanzania
May 7, 2005
May 7, 2005 at 8:42 pm
Não percebo nada do que está aqui escrito, mas parece-me uma língua muito melodiosa!
May 8, 2005 at 5:23 am
Nimefurahia sana blogi yako na mada zake za kuvutia. Umefanya vyema kuamua kufahamisha watu kuhusu Tanzania kwani vyombo vya habari vya ng’ambo vimejaa porojo tu kuhusu bara Afrika.
Lo, hata huyo hapo juu asiyeongea Kiswahili asema amependezwa sana na lugha hii:))
Makuu haya, hata kama ameandika Kireno cha Brazil
May 8, 2005 at 8:13 pm
Hapa umecheza. Hongera. Nadhani bodi ya utalii itabidi wakulipe!!!!!!!!
May 9, 2005 at 10:23 am
@anonymous
Thubutu, wangekuwa na hela za kulipia wangeshatangaza utalii tulio nao zamani sana, inabidi kujitolea kwa mapenzi yetu kuitangaza nchi yetu