Kwa hakika kikao cha ‘Baraza la makadinali wa CCM’, kilichokutana kwa muda wa siku tatu mjini Dodoma, kimefanikiwa kumpata ‘Papa’ wao, ambaye atakiongoza chama hicho kuibuka, kwa mara nyingine tena, na ushindi wa kishindo, katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2005. Soma hapa kumjua huyo ‘Papa mtakavitu’. Ikiwa unalolote unalopenda kujadili kuhusu mshindi huyu, bilashaka wakati ni huu, karibu tumjadili.
May 5, 2005
May 6, 2005 at 5:26 pm
Kweli moshi ulifuka na tumempata bila shaka raisi wa kufaa.Mimi nilitabiri katika makala yangu wiki jana eti Sumaye angeshinda lakini wapi.
Hebu niaelezwe ilikuwaje akashindwa au mizengwe?
May 6, 2005 at 6:44 pm
@ Kessy Inno.
Ndugu yangu, hakuna mizengwe katika dunia hii, tatizo kubwa ambalo linatukabili Watanzania ni kwamba hatuna utaratibu wa kuelezana ukweli pale inapobidi tufanyiane hivyo. Kama kuna vitu ambavyo Mwalimu aliwahi kufeli enzi za uhai wake ndani ya chama, basi hili linaweza kuwa moja wapo. Kushindwa kujenga mfumo mzuri wa kuelezana ukweli pale inapotakiwa. na matokeo yake unajua yalikuwa ni nini kaka? Neno MIZENGWE. Kwa faida yako na ya wengine nimeamua kuandika makala kuhusiana na hili naamini ukiisoma utanielewa ndugu yangu