Kwa kadiri ambavyo tumekuwa tukielekea kuukaribia uchaguzi mkuu nchini Tanzania, ndivyo ambavyo wananchi wakekuwa wakijiluza maswali kadhaa kuhusiana na uchaguzi huo na hasa kuwahusu wale ambao wamekuwa wakiwania kutuongoza wakati rais, Benjamin William Mkapa, atakapomaliza muda wake.

Hakuna hata mmoja kati ya wanaowania nafasi hiyo, ambaye amekubali kuwa aliwahi kuwa au kwa sasa ana mapungufu ya aina yoyote ile, hili likimaanisha kuwa, kila mmoja ni Mtakatifu. Hata hivyo, wakati wao wakitushurutisha tuamini hivyo, baadhi ya wananchi nikiwemo mimi binafsi, najiuliza maswali mengi kuhusiana nao.

Miongoni mwa maswali ambayo nimekuwa nikijiuliza ni hili: Hivi kweli, kwa mambo haya wanayotufanyia au walioyafanya, tutaweza kweli kumpata Rais ambaye ni Mtakatifu au tutampata aliye Mtakavitu? Yasome mawazo yangu hapa.