Kwa kadiri ambavyo tumekuwa tukielekea kuukaribia uchaguzi mkuu nchini Tanzania, ndivyo ambavyo wananchi wakekuwa wakijiluza maswali kadhaa kuhusiana na uchaguzi huo na hasa kuwahusu wale ambao wamekuwa wakiwania kutuongoza wakati rais, Benjamin William Mkapa, atakapomaliza muda wake.
Hakuna hata mmoja kati ya wanaowania nafasi hiyo, ambaye amekubali kuwa aliwahi kuwa au kwa sasa ana mapungufu ya aina yoyote ile, hili likimaanisha kuwa, kila mmoja ni Mtakatifu. Hata hivyo, wakati wao wakitushurutisha tuamini hivyo, baadhi ya wananchi nikiwemo mimi binafsi, najiuliza maswali mengi kuhusiana nao.
Miongoni mwa maswali ambayo nimekuwa nikijiuliza ni hili: Hivi kweli, kwa mambo haya wanayotufanyia au walioyafanya, tutaweza kweli kumpata Rais ambaye ni Mtakatifu au tutampata aliye Mtakavitu? Yasome mawazo yangu hapa.
April 24, 2005 at 3:03 pm
Nimependa makala, hasa neno “mtakavitu.”
April 28, 2005 at 1:13 pm
Taarifa na mawazo murua. Naunga mkono rushwa na utakavitu ni tabia, wala si hulka ya ghafla
May 1, 2005 at 2:55 pm
Lakini unadhani ni wangapi wanajua au kukubaliana na hilo? Wapo wengi ambao hawataki lakini hili naamini limetokana na kutokuwepo kwa mfumo mzuri wa kuelezana ukweli, ndio maana ukimwambia mtu ukweli unaambiwa unamfanyia Mizengwe–>